FOR ALL INSURANCES AND AGRICULTURE INPUTS
Sprayer pump- Ni vifaa maalum vinavyo tumika kunyunyizia viuatilifu(sumu) kwenye mazoa ili kudhibiti visumbufu vya mazoa. Mabomba yametengenezwa kwa kukidhi mahitaji mbalimbali ,mabomba haya yana Nozeli sahihi ambazo zinatoa matone sahihi na yanayo fika kwenye kisumbufu lengwa .
Kampuni yetu mtewele general traders tunauza na kusambaza mbegu za mazao mbalimbali mahindi ,soya,Alizeti,mbegu ya mbogamboga za makapuni mbalimbali. Kwa upande mmbegu za mahindi tuna zinazo komaa kuanzia siku 135-150 mfano PAN 691,SC 719,UH 6303 ,pia tuna za muda mfupi kama SC 403 & 419. Mbegu za mbogamboga-Tunauza na kusambaza mbegu zenye ubora zinazo vumilia magonjwa eg Vitunguu ,kabichi,nyanya ,karoti,Figiri,Hoho n.k.
Viua kuvu:-Ni viuatilifu vinavyo dhibiti kuvu kwenye mazao ,viua kuvu kuna vinavyo zuia/preventive na vinavyo tibu/curative. Vinavyo zuia/preventive-Hivi ni viuatilifu vinavyo fanya kazi ya kuzuia mazao yasishambuliwe na mara nyingi hutumiwa hata kama hujaona dalili za ugonjwa shambani Mfano ; Farmzeb 80 WP(Mancozeb) ,Z-force( Mancozeb),Chloroforce (Chlorothalonil ) ,ebony (Mancozeb) n.k.
VIUA GUGU-Ni viuatilifu vinavyo tumika kwenye palizi na kusafisha mashamba. Viuatilifu hivi vimegawanyika kwenye makundi kadhaa Pre –emergence/Vinatumika kabla ya magugu au zao kuota mfano Sure start na Primagram hutumika kuzuia magugu kuota kwenye mahindi na hutumika baada ya kupanda mahindi.
VIUA DUDU/INSECTICIDES-Ni sumu inayotumika kuua,kufukuza wadudu wanao shambulia mazo shambani au gharani.Viua dudu vinajulikana kama Viuatilifu ambavyo vina kiambata amilifu ambacho ndicho kinafanya kazi ya kuua,kufukuza na kuzuia mazao yasishambuliwe na visumbufu,mfano wa visumbufu wadudu,magonjwa na magugu.
Ni mbolea ambazo hutumika kunyunyizia kwenye majani ya mazao husika kwa lengo la kuchochea ukuaji na kuboresha mavuno.Mbolea hizi huchanganywa na maji kwa kiwango ambacho kinakubarika.
Mbolea za kukuzia;Ni mbolea zenye kiwango kizuri cha kirutubisho cha Naitrojeni (N) ambacho kazi yake kubwa ni kuupa mmea ukijani kibichi ili mmea uweze kujitengenezea chakula chake na kuufanya mmea kukamilisha mzungunguko wake wa maisha.Mfano wa mbolea hizi ni :-
Mbolea za kupandia;Ni mbolea zenye kiwango kizuri cha kirutubisho cha Fosforasi (P) ambacho kazi yake kubwa ni kuchochea ukuaji wa mizizi ili iweze kuchukua chakula(virutubisho) na maji kwenye udongo.Mfano wa mbolea hizi ni :-